Lampard apigwa kalamu Chelsea
25 Januari 2021Matangazo
Katika msimu wake wa kwanza aliisaidia Chelsea kumaliza katika mojawapo ya nafasi za Champions League ila kwa kuwa klabu hiyo inashikilia nafasi ya 9 kwenye msimamo kwa sasa, mmilki Roman Abramovich amelazimika kuchukua hatua.
Chelsea imesema haitatoa taarifa nyengine yoyote hadi pale mrithi wa Lampard atakapotangazwa. Wachambuzi wanasema kocha wa zamani wa Borussia Dortmund na PSG Thomas Tuchel ndiye anayetarajiwa kuichukua nafasi hiyo.