Ungana na Fathiya Omar katika makala ya Vijana Tugutuke, ambako vijana mbalimbali wa Mombasa wanazungumzia kuhusu kuongezeka kwa mimba za utotoni mjini humo. Wakati huu wa janga la virusi vya corona watoto wengi wamepewa mimba, huku kampeni mbalimbali za kuzuia mimba za utotoni nchini Kenya zikiendelea.