Mkoa wa kivu kusini unashuhudia ongezeko la visa vya ugonjwa wa Covid-19 katika eneo hilo. Gavana wa mkoa huo ametangaza kwamba watu 3 wamefariki kutokana na ugonjwa huo huku watu wapatao 100 wanashukiwa kuambukizwa ugonjwa huo mjini Bukavu na tangu leo mji huo utafungwa tena kwa wiki mbili. Kutoka Bukavu, Mitima Delachance alituarifu.