Makala Yetu Leo inaangazia shughuli ya wapiga debe katika vyombo vya usafirishaji abiria nchini Tanzania. Je, kuna umuhimu ama ulazima wa kuwepo wapiga debe? Kwa nini watu hawa wamekuwepo kwa muda mrefu wakifanya shughuli hii? Na je wapiga debe hawa wanatambulika katika mamlaka husika? Jamii inazungumzia nini hasa kuwepo kwa wapiga debe? Msimulizi ni Deo Kaji Makomba kutoka Dodoma.