Tani milioni mbili za mkaa hutumika kila mwaka katika mji mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Kinshasa, kupikia na kupasha maji moto, lakini matokeo yake ni kuangamia kwa misitu asilia ya taifa hilo la pili kwa misitu mikubwa duniani. Kurunzi inaangazia juhudi za kupambana na hali hii.