Ungana na Amina Abubakar katika kipindi cha Afya Yako ambapo anauangazia ugonjwa wa kichaa cha mbwa ambao mtu huupata pale anapong‘atwa na mbwa anayeugua ugonjwa huo. Kichaa hicho cha mbwa, ni ugonjwa hatari ambapo asilimia 99 unaenezwa na mbwa baada ya kumng’ata binaadamu, kumramba au hata kumkwangua kwa kucha zake.