Michuano ya Euro 2022 kwa wanawake: Timu za kutizamwa
Ufaransa
Baada ya kushindwa katika kombe la dunia la 2019 nyumbani, kikosi cha Corinne Diacre kitataka kujiimarisha. Inaweza kuwa vigumu kutokana na kukosekana kwa wachezaji mahiri kama vile Amandine Henry na Eugenie Le Sommer, ambao wameachwa kwenye kikosi. Beki mwenye uzoefu Wendie Renard, wa mabingwa watetezi wa Champions League Lyon, anaongoza timu yenye uzoefu mwingi wa ushindi katika ngazi ya klabu.