Mwanzoni mwa 2017, Edith Kimani aliondoka kuja Ujerumani kuanza maisha mapya na kazi mjini Berlin, kama mtangazaji wa habari wa DW. Aliacha mashabiki wengi nchini Kenya lakini alileta uzoefu wa miaka saba kama ripota na mtangazaji wa habari wa moja ya vituo vikubwa kabisa vya televisheni nchini Kenya, KTN.