Chama cha Democrats kimepata ushindi wa kishindo katika baraza la wawakilishi na kukiacha hoi chama cha Republican ambacho kimebakia na ushindi wa baraza la Seneti.Matokeo hayo yanaonesha nguvu za Democrats zimerejea upya katika siasa za Marekani tangu alipoingia madarakani Donald Trump ambaye sasa huenda akakabiliwa na wakati mgumu katika ikulu ya White House.