1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaMarekani ya Kusini

Cuba yaanza kuwaachia maelfu ya wafungwa

4 Aprili 2026

Mamlaka za Cuba zimeanza kuwaachilia wafungwa baada ya kutangaza kuwa nchi hiyo itatoa msamaha kwa wafungwa 2,010. Hii ni mara ya pili ndani ya kipindi cha chini ya mwezi mmoja.

https://p.dw.com/p/5Bek2
Wafungwa nchini Cuba
Wafungwa katika gereza nchini Cuba, Aprili 9, 2013Picha: Franklin Reyes/AP/picture alliance

Zaidi ya wafungwa 20 waliachiliwa kutoka gereza la La Lima mashariki mwa Havana, wakiwa wameshikilia nyaraka zao za kuwa huru, wakilia na kuwakumbatia jamaa zao ambao walikuwa wakiwasubiri tangu asubuhi.

Haijajulikana hadi sasa ikiwa wale walioachiliwa Ijumaa ni wafungwa wa kisiasa, kwani hakuna orodha iliyochapishwa. Mamlaka za Cuba zinakana kuwashikilia wafungwa wa aina hiyo.

Wizara ya mambo ya nje ya Marekani imesema inafahamu taarifa kuhusu kuachiliwa kwa wafungwa, lakini ikaongeza kuwa haijulikani wazi kama wafungwa wowote wa kisiasa watakuwa miongoni mwao.