BERLIN:Rais Köhler kuamua iwapo atagombea wadhfa wake
25 Juni 2007Matangazo
Rais wa shirikisho la Jamuhuri ya Ujerumani Horst Köhler hajaondoa uwezekano wa kupigania tena wadhfa wake ifikapo mwaka wa 2009.
Akihojiwa katika kipindi cha televisheni cha ARD – Sabine Christiansen rais Köhler amesema ataamua mwaka mmoja kabla ya muhula wake wa sasa kumalizika.
Rais Horst Köhler mnamo Julai mosi atakamilisha miaka mitatu tangu akabidhiwe wadhfa huo wa juu wa heshima nchini Ujerumani.
Wakati huo huo rais Köhler ametetea hoja ya rais wa shirikisho kuchaguliwa moja kwa moja na raia.