Arsenal yaongoza nane bora kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya
29 Januari 2026
Matangazo
Kocha wa Arsenal ambayo kwa sasa inashika usukani Mikel Arteta amesifu kiwango cha kikosi chake walichoonyesha kwenye hatua hii ya awali ya michuano hiyo.
Kairat inayoshiriki kwa mara ya kwanza imemaliza ikiwa nafasi ya mwisho kwenye orodha ya timu 36 ikiwa na pointi moja tu, baada ya mechi hizo nane.
Kwa upande mwingine, mshambuliaji wa Real Madrid, Kylian Mbappe amekiri kwamba timu yake haikuwa katika nafasi nzuri, na kushindwa kuingia kwenye nane bora, baada ya kichapo cha 4-2 dhidi ya Benfica ya Jose Mourinho.
Madrid mabingwa mara 15 wa Champions, sasa watalazimika kucheza mechi ya kufuzu ili kusonga mbele.