1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Arsenal mabingwa wa FA Cup England

Sekione Kitojo
2 Agosti 2020

Arsenal imefanikiwa kutwaa taji la kombe la FA nchini England baada ya kuwaangusha mahasimu wao wa mjini London Chelsea kwa  mabao 2-1 jana Jumamosi katika  uwanja wa Wembley katika fainali  ya 139 ya kombe hilo.

https://p.dw.com/p/3gHen
Fußball I Arsenal v Chelsea
Picha: picture-alliance/C. Ivill

Alikuwa  mshambuliaji Pierre  Emerick Aubameyang  ambaye anahusishwa  na  tetesi  za  kutaka  kuihama  timu  hiyo, aliyepachika  mabao  yote  mawili  muhimu  kwa  ushindi  wa Arsenal. Muda pekee  ambao  Pierre-Emerick  Aubameyang alionekana  kutokuwa  na  uhakika  ni  wakati  ulipowadia  kuchukua kombe  hilo  la  FA.

Fußball I Arsenal v Chelsea
Pierre Emerick Aubameyang akifunga bao la kusawazisha dhidi ya Chelsea Picha: picture-alliance/C. Ivill

Mabao mawili kutoka  kwa  mshambuliaji  huyo  yalibadilisha muelekeo  wa  fainali  hiyo  kwa  Arsenal  na  kufanikisha  ushindi wa  mabao 2-1  dhidi  ya  Chelsea siku  ya  Jumamosi  katika  fainali ya  kwanza  ya  kombe  hilo iliyochezwa  bila  mashabiki.

Vizuwizi  kutokana  na  virusi  vya  corona  vilikuwa  na  maana hakukuwa  na  mwanamfalme William  katika  uwanja  wa  Wembley kukabidhi kombe  hilo  katika kizimba cha  mfalme  katika  uwanja huo maarufu duniani.

Kwa  hiyo Aubameyang alilazimika  kuchukua  kombe  hilo  binafsi uwanjani  hapo  akiwa  kama  nahodha wa  timu. Kwa kuchukua kitako cha  kombe  hilo pia, kilisababisha  Aubameyang  kudondosha kombe  hilo.

"Nilimuona  akitembea  akiwa  amechukua  pia  sehemu  ya  chini  ya kombe  hilo," mlinzi  wa  Arsenal Rob Holding alisema, "na ilikuwa kama, "Unahitaji kuondoa  sehemu hiyo ya chini !"

Coronavirus in Premierleague FC Arsenal Trainer Mikel Arteta
Kocha wa Arsenal Mikel Arteta amenyakua taji lake la kwanza tangu kujiunga na Arsenal kama kochaPicha: AFP/G. Kirk

Kombe  hilo lilinyanyuliwa  juu , wakati vikimwagika vikaratasi vya rangi ya dhahabu kwa kikosi  hicho  cha  Arsenal katika  uwanja ambao  ulikuwa  mtupu uwanja  ambao  una  uwezo wa  kusheheni mashabiki  90,000 baada  ya  fainali  hiyo  ya  139  ya  mashindano hayo ya muda  mrefu  zaidi  duniani  katika  mchezo  wa  kandanda.

Mwandishi: Sekione Kitojo / ape