1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Annan kwenda Syria haraka

28 Mei 2012

Mjumbe wa Arab League na umoja wa mataifa nchini Syria Kofi Annan anakwenda kwa ziara yake ya pili mjini Damascus akitafuta njia za kuweka uhai katika mpango wake wa amani ,kufuatia mauaji ya kinyama nchini Syria.

https://p.dw.com/p/153O9
epa03237299 A handout picture released by the Syrian Arab News Agency (SANA) shows members of the UN observers Mission in Syria during their visit to Duma in out-skirts Damascus, Syria, 26 May 2012. The UN observers confirmed after visiting a town in central Syria, that 92 people had died there - among them 32 children - in what activists said was shelling by government forces. The rebel opposition Free Syrian Army (FSA) called on the UN to meet its responsibilities and stop the violence in Syria. Otherwise, it said, the group could no longer commit to the ceasefire brokered by UN-Arab League envoy, Kofi Annan. EPA/SANA HANDOUT
Kikosi cha umoja wa mataifa kinachoangalia makubalianoPicha: picture-alliance/dpa

Mauaji ya kinyama ya zaidi ya watu 100 nchini Syria yanaweza kuwa ni mwanzo wa kuwaweka katika njia panda rais Bashar al-Assad na mpatanishi wa kimataifa Kofi Annan. Wanadiplomasia wanasema ishara sio nzuri kwa juhudi za kila upande.

Baraza la usalama la umoja wa mataifa jana lilishutumu vikali kuhusika kwa serikali ya Syria katika mashambulizi ya makombora dhidi ya kijiji cha Houla . Taarifa yake hata hivyo haikuweza kuyaleta mataifa makubwa duniani pamoja katika azma ya kufikisha mwisho mzozo huo.

The Joint Special Envoy for Syria, Kofi Annan waits for Nassir Abdulaziz Al-Nasser (not pictured) President of the 66th session of the U.N. General Assembly before a meeting at the United Nations European headquarters in Geneva May 8, 2012. Syria is finding it increasingly hard to buy grain on international markets because sanctions have blocked its access to trade finance, while growing numbers of its citizens are struggling to obtain food after more than a year of conflict. A confidential United Nations aid document obtained by Reuters showed at least 1 million Syrians need humanitarian aid. REUTERS/Denis Balibouse (SWITZERLAND - Tags: POLITICS HEADSHOT)
Mjumbe maalum wa umoja wa mataifa na Arab League Kofi AnnanPicha: Reuters

Marekani yashutumu

Marekani na mataifa ya Ulaya , wamesema kuwa mauaji hayo ni ishara mpya ya jinsi utawala wa Assad ulivyo wa kinyama. Ushahidi ni wazi na kuna ishara kamili ya uhusika wa serikali katika mauaji haya, amesema Peter Wittig , balozi wa Ujerumani katika umoja wa mataifa.

Urusi inapinga ushahidi huo na kuendelea kuikingia kifua nchi hiyo mshirika wake wa karibu katika mashariki ya kati.

Hatuamini kuwa serikali ya Syria itapendelea kuharibu ziara ya mjumbe maalum Kofi Annan , ziara ambayo ni muhimu sana ambapo tunatarajia mengi ya maendeleo, amesema Igor Pankin, naibu balozi wa Urusi katika umoja wa mataifa.

Urusi yalaumu waasi

Urusi na serikali ya Syria zinaendelea kuyalaumu makundi ya upinzani pamoja na watu kutoka nje wenye misimamo mikali kwa kuleta ghasia nchini humo. Waziri wa mambo ya kigeni wa Uingereza William Hague amesema kuwa hii ni mbinu ya muda mrefu sasa ya serikali ya Syria.

"Hii ni mbinu inayofahamika ya utawala wa Assad ya kuwalaumu watu wengine kwa kile kinachotokea nchini mwake, ili kujaribu kujitoa katika wajibu kwa kiwango cha mauaji na uharibifu. Tumechukizwa sana katika serikali ya Uingereza na katika jumuiya ya kimataifa kwa kile tulichokiona katika muda wa siku chache zilizopita, hususan vifo vya zaidi ya watu 100 ambao hawakujihami kwa silaha , wanaume, wanawake na watoto".

Jeshi huru la Syria pamoja na waasi wengine wakati huo huo wanasema kuwa mauaji ya Houla ni sababu nyingine kwanini hawataheshimu kusitisha mapigano ambayo yamepatanishwa na Kofi Annan lakini ambayo hayajafanyakazi.

Wataalamu wa mataifa ya magharibi wanasema kuwa Assad huenda ataendelea kuwapo madarakani kwa miezi kadha, kama sio muda mrefu zaidi. Wakati waangalizi wa makubaliano ya kusitisha mapigano wa umoja wa mataifa nchini Syria , tayari wanashambuliwa na ghasia zinaongezeka , kuna matumaini finyu ya juhudi za amani za Kofi Annan .

Mauaji ya kuchukiza

Mkuu wa ujumbe wa umoja wa mataifa nchini Syria meja jenerali Robert Mood amesema kuwa mauaji hayo ni ya kuchukiza.

The head of the U.N. observer mission to Syria, Maj. Gen. Robert Mood, speaks to reporters after a roadside bomb attacked a Syrian military convoy, in Daraa city, southern Syria, Wednesday, May 9, 2012. Mood said he does not know whether the blast was meant to target the observers or the military. (Foto:Muzaffar Salman/AP/dapd).
Mkuu wa ujumbe wa UN nchini Syria Robert MoodPicha: dapd

"Haisameheki . Vifo vya watoto zaidi ya 50, hali ya baadaye ya Syria , ni kitu ambacho kinasikitisha sana".

Mpango wa Annan haujakufa, amesema balozi wa Uingereza katika umoja wa mataifa Mark Lyall Grant. Lakini katika mazungumzo kuhusu mashariki ya kati kesho Jumanne na Syria siku ya jumatano baraza linahitajika kuwa na mkakati maalum wa majadiliano juu ya mpango wa Annan na kile baraza hilo la amani linaloweza kufanya kumsaidia mjumbe huyo mpango wake kufanyakazi.

Wakati huo huo kundi la wapinzani limesema leo kuwa mashambulio ya jeshi la serikali ya Syria yamesababisha mauaji ya watu 41 katika mji wa Hama katika muda wa saa 24 zilizopita.

Mwandishi : Sekione Kitojo / afpe /rtre

Mhariri: Hamidou Oummilkheir