Kwenye Maoni Mbele ya Meza ya Duara, Mohammed Khelef anaongoza mjadala juu ya nafasi ya aliyekuwa Waziri Mkuu wa Tanzania, Edward Lowassa, katika siasa za mageuzi nchini humo, hasa baada ya kuhamia kwake kwenye kambi ya upinzani na kutangaza nia ya kuwania urais kupitia jukwaa la Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA).