Hatua za kushitukiza na kushangaza za rais mpya wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Pombe Magufuli, zinazodhamiria kurejesha moyo wa uwajibikaji kwenye sekta ya umma sio tu zimezaa msamiati wa "umagufulishaji", bali pia maswali makubwa ya ikiwa zitadumu na zitaibadilisha nchi iliyozama kwenye ufisadi, ubadhirifu na uholela wa muda mrefu.