Juhudi za kuwafukua waliosalimika na zilzala nchini Peru zinaendelea
18 Agosti 2007Matangazo
Lima
Waokoaji wanaendelea kuchunga na kupekua magofu ya majumba kuwasaka walionusurika na zilzala iliyopiga jumatano iliyopita nchini humo.Zilzala hiyo imegharimu maisha ya zaidi ya watu 500.Rais Alan Garcia ameweatolea mwito wananchi waliokumbwa na maafa hayo wasubirie.Ameongeza kusema serikali yake itachukua hatua ya kupambana na wanaopora mali.Kabla ya hapo ripoti za radio nchini humo zilizungumzia juu ya watu waliowavamia madareva wa malori na kupora mali,bila ya polisi kuingilia kati.