Virusi vya ugonjwa wa miguu na midomo vimetokea maabara
5 Agosti 2007Matangazo
Kwa maoni ya wataalamu,virusi hivyo vimetokea maabara ya kampuni hiyo na kuwaambukiza ngombe katika shamba lililo umbali wa kiasi ya kilomita sita.
Serikali ya Uingereza,imeamaua kwa hiyari kupiga marufuku usafirishaji wa mifugo na bidhaa za wanyama.Hali ya wasiwasi pia imeufanya Umoja wa Ulaya,kupiga marufuku kuagizia mifugo kutoka Uingereza.
Waziri Mkuu wa Uingereza Gordon Brown amesema, serikali itachukua hatua za haraka kudhibiti ugonjwa huo.
Mripuko wa ugonjwa wa miguu na midomo katika mwaka 2001 ulipelekea kuua mifugo milioni 7 na uliathiri vibaya sana sekta za kilimo na utalii.