1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Viongozi wa kundi la FDLR wakamatwa nchini Ujerumani.

Sekione Kitojo17 Novemba 2009

Polisi wa Ujerumani wamewatia nguvuni viongozi wawili wa kihutu ambao wameongoza harakati za waasi nchini humo.

https://p.dw.com/p/KZFC
Wakishiriki kwa pamoja ujenzi mpya wa nchi yao vijana wa Rwanda Wahutu na Watutsi kutoka katika kundi la vijana la kuondoa mauaji ya kimbari wanafanyakazi kwa pamoja kuhamasisha watu kuishi kwa amani.Picha: Christine Harjes

Kalsruhe :

Polisi ya Ujerumani imewatia nguvuni viongozi wawili wa Kihutu ambao wameongoza harakati za waasi wanaoendesha visa vya ubakaji, mauaji na uharibifu mashariki mwa Congo.

Dr Ignace M mwenye umri wa miaka 46 ambaye ni rais wa kundi la waasi la FDLR anatakiwa nchini Rwanda kwa uhalifu wa kivita.

Maafisa wa Ujerumani wanalichukulia kundi hilo kuwa la kigaidi.

Mwingine aliyekamatwa ni Naibu wake anayejulikana kwa jina la Straton M mwenye umri wa miaka 48.

Mwendesha mashitaka wa Shirikisho alisema kuna ushahidi wa kutosha kuwa, wanahusika na uhalifu wa kivita.

Huenda wakafunguliwa mashtaka hapa Ujerumani.