1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Umoja wa Ulaya watoa msaada wa fedha kwa Afrika

18 Julai 2008

Umoja wa Ulaya umeliahidi bara la Afrika msaada wa euro bilioni moja kuimarisha sekta ya Kilimo.

https://p.dw.com/p/Eesw
Kamishna wa Jumuiya ya Ulaya Bw.Louis Michel atoa ahadi ya msaada barani Afrika.Picha: AP

Lengo la hatua hiyo ni kuliwezesha bara hilo kukimu mahitaji yake ya chakula.Ahadi hiyo ilitolewa hapo jana jioni mjini Dar es Salaam nchini Tanzania wakati wa kikao cha siku mbili kinachojadilia ushirikiano wa kikanda kati ya eneo la Afrika mashariki na Kusini vilevile eneo la bahari ya Hindi.

Mwandishi wetu wa Dar es Salaam Pascal Mayala alihudhuria kikao hicho na kuandaa taarifa ifuatayo.