Baada ya mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali, Prof. Mussa Assad kutoa ripoti yake ya ukaguzi wa mapato na matumizi ya fedha za umma kwa mwaka wa fedha wa 2016/17, mjadala umezuka juu ya masuala nyeti ikiwa ni pamoja na upotevu wa shilingi trilioni 1.5 na matumizi mabaya ya fedha. DW imezungumza na mchambuzi wa uchumi Hamduni Marcel na kwanza anatoa tathmini yake kuhusu ripoti hii.