1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Polisi wauawa na wanamgambo nchini Irak

22 Novemba 2007
https://p.dw.com/p/CS19

Hadi watu 10 wameuawa kusini mwa mji mkuu wa Irak,Baghdad.Wanamgambo wanaoshukiwa kuhusika na al-Qaeda waliwaua polisi 8 waliokuwa wakipiga doria.Hapo kabla waliwapiga risasi wanajeshi 2 wa Kiiraki na kuwanyanganya gari lao.Wanamgambo hao walifyatua risasi katika mtaa wa Hawr Rajab kusini mwa Baghdad wanakoishi Wairaki wengi wa madhehebu ya Kisunni na ni ngome ya al-Qaeda. Viongozi wa makundi ya kikabila ya madhehebu ya Kisunni,wamekuwa wakiwajumuisha wanaume vijana katika vikosi vya polisi katika jitahada ya kuwatimua wafuasi wa al-Qaeda.