1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Miripuko yauwa watu 40 na kujeruhi 150 Iraq

13 Desemba 2007
https://p.dw.com/p/CbC4

BAGHDAD

Mabomu matatu yameripuka kwa haraka moja baada ya jengine katika soko kuu kwenye mji wa kusini wa wakaazi wa madhehebu ya Washia na kuuwa watu 41 na kujeruhi wengine 150.

Hilo ni shambuli baya kabisa dhidi ya raia wa Iraq kuwahi kushuhudiwa katika kipindi che miezi mine.

Miripuko hiyo ya maafa hapo jana katika mji wa Amara wenye kuzalisha mafuta ambao ulikuwa kwa kiasi kikubwa haukukumvwa na uwagaji damu wa kikabila umetokea siku chache tu baada ya Uingereza kutarajiwa kukabidhi kwa vikosi vya Iraq jimbo la kusini mwa nchi hiyo ambalo ni la mwisho kuwa chini ya udhibiti wa vikosi vya Uingereza tokea kuvamiwa kwa nchi hiyo hapo mwaka 2003.