Miaka minane tangu kufariki dunia Mwalimu Julius Nyerere wa Tanzania
15 Oktoba 2007Licha ya kwamba mafundisho ya marehemu Julius Nyerere juu ya siasa ya ujamaa na kujitegemea sasa hayatekelezwi, kinyume na ilivokuwa pale alipokuwa madarakani, hata hivyo Watanzania wanapobishana katika masuala mbali mbali hurejea nyuma na kumkumbuka Mwalimu Nyerere kama kituo cha uadilifu, na hasa ile ndoto isiotimia bado ya kuwatupia jicho la huruma watu wa tabaka la chini.
Ni Othman Miraji wapendwa wasikilizaji katika makala haya ya DARUBINI, uchambuzi wa kisiasa wa kila wiki kutoka Radio Deutsche Welle, mjini Bonn, Ujerumani.
Hebu kwanza tuyadurusu matamshi ya Mwalimu Nyerere tuliyoyapata katika maktaba yetu. Akizungumzia juu ya siasa ya Ujamaa na Kujitegemea, jaribio ambalo wachunguzi wanasema lilikuwa na nia nzuri , lakini lilishindwa kuleta matarajio yaliowekewa:
Insert: Nyerere 1 Ujamaa na Kujitegemea
Mwalimu anasifiwa kuwa muasisi wa Muungano wa Tanganyika na Visiwa vya Zanzibar uliozaa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Alikuwa mkakamavu juu ya muungano huo na kuyapuunza matakwa ya baadhi ya watu waliotaka ipigwe kura ya maoni kuwauliza watu wa sehemu mbili za Muungano kama wanaukubali…
Insert:: Nyerere 2 Muungano wa Tanzania…
Hayati Mwalimu Nyerere pumzi zake pia alizielekeza kutaka Bara la Afrika liwe na Umoja, mfano wa Umoja wa Ulaya ulimvutia…
Insert: Nyerere 3 Umoja wa Afrika….
Kuyajua zaidi yale yaliofanywa na Hayati Mwalimu Nyerere wakati wa uhai wake, mwandishi wetu wa Dar es Salaam, Hawra Shamte, ameandaa yafuatayo:
Insert: Mwalimu Revisited
Na kwa hayo kutoka kwa mwandishi wetu wa Dar es Salaam, Hawra Shamte, aliyeukumbuka mwaka wa nane tangu muasisi wa taifa la Tanzania, Mwalimu Nyerere, kufariki, tunakamilisha makala haya ya DARUBINI, uchambuzi wa kisiasa wa kila wiki kutoka Radio Deutche Welle, Bonn, Ujerumani. Hadi mara nyingine…