1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kocha Loew ataja kikosi cha Die Mannschaft

Sekione Kitojo
4 Juni 2018

Kikosi cha timu ya taifa ya Ujerumani Die Mannschaft chatangazwa, mshambuliaji wa Manchester City Leroy Sane aachwa.

https://p.dw.com/p/2yv9e
Fußball: WM-Qualifikation Nationalmannschaft Joachim  Jogi Löw
Picha: picture alliance/GES/M. Gilliar

Wakati  macho  na  masikio  ya  wapenzi  wa  kandanda duniani  yanaelekezwa  nchini  Urusi. Vikosi  mbali  mbali rasmi  vya  timu  zinazoshiriki  katika  fainali  hizo vinatangazwa  leo  kwa  matayarisho  ya  mwisho  kabla  ya michuano  hiyo  kung'oa nanga  hapo  Juni  14  siku  10 kuanzia  sasa. Ujerumani ikiwa  ni  mabingwa  watetezi  wa kombe  la  dunia  imetangaza  pia  kikosi  chake  rasmi.

Leroy Sane
Leroy SanePicha: picture-alliance/GES/augenklick/M. Ib

Mchezaji  wa  kati  mshambuliaji  kutoka  klabu  ya Manchester City  Leroy Sane  atakosekana  katika  kikosi cha  mwisho  cha  kocha  Joachim Loew  cha timu  ya  taifa ya  Ujerumani  Die  Mannschaft  kwa  ajili  ya  fainali  za kombe  la  dunia  kwa  mujibu  wa  taarifa  leo wakati mlinda  mlango Manuel Neuer alitajwa  miongoni  mwa wachezaji  23 wanaokwenda  Urusi  kutetea  ubingwa  huo.

Neuer  alijumuishwa  katika  kikosi  hicho  licha  ya kucheza  katika  mchezo  mmoja  tu  rasmi , mchezo  wa kirafiki  dhidi  ya  Austria  siku  ya  Ijumaa, tangu alipovunjika  mfupa  mdogo wa  nyuma  wa  mguu  wake mwezi  Septemba  mwaka  jana  lakini  mchezaji  mwenye kipaji Sane  mwenye  umri  wa  miaka  22  ni  jina  kubwa ambalo  halimo  katika  orodha  hiyo.

Mchezaji  huyo  wa  Manchester City, mlinda  mlango Bernd Leno, mshambuliaji Nils Petersen na  mlinzi Jonathan Tah ni  wachezaji  wanne  ambao  wameshindwa kumshawishi  kocha  Joachim Loew  kwamba  wanaweza kuisaidia  timu hiyo  katika  fainali  za  kombe  la  dunia.

Jonathan Tah
Jonathan TahPicha: picture-alliance/Revierfoto

Loew  alitangaza  kikosi  chake  mwishoni  mwa  kambi  ya mazowezi  katika  milima  ya  Alps  nchini  Italia. Ujerumani itacheza  mchezo  wake  wa  mwisho  wa  matayarisho dhidi  ya  saudi  arabia  mjini  Leverkusen  siku  ya  Ijumaa kabla  ya  kuanza  kwa  mashindano  hayo  Juni  14.

Nae kansela  wa  Ujerumani  Angela  Merkel aliwatembelea wachezaji  wa  timu  hiyo  ya  taifa  jana  Jumapili  na kuzungumza  nao  juu  ya  uzoefu  wake   kuhusu  Urusi kabla  ya  kikosi  hicho  kutangazwa  rasmi  leo. Baada  ya chakula  cha  jioni  katika  hoteli  katika  jimbo  la  kusini nchini  Italia  la  Tyrol , Merkel , ambaye  huzungumza ugha  ya  kirusi  bila  matatizo baada  ya  kukulia  katika iliyokuwa  Ujerumani  mashariki  ya  zamani , alikiambia kikosi  hicho  juu  ya  nchi  hiyo  na  watu  wake, meneja wa  timu  hiyo Oliver Bierhoff  alisema.

WM 2018 - Trainingslager Deutschland - Merkel
Kansela Merkel akizungumza na wachezaji wa timu ya taifa mjini Appen, jimboni Tyrol nchini ItaliaPicha: picture-alliance/dpa/Bundesregierung/G. Bergmann

"Tumefarijika  sana  kwamba  aliweza  kuchukua  muda wake  na  kukutana nasi. Bila  shaka  ziara  ya  kansela  ni muhimu kila  wakati. Na  ilikuwa  sio ziara  rasmi, na  alipata fursa  ya  kuzungumza  na  wachezaji. Lakini  si  hayo  tu, bali  pia  kansela  anaifahamu  vizuri Urusi  na alizungumzia  kuhusu  nchi  hiyo  na  watu  wake  na  pia kuhusu  maoni  yake  kuhusu Urusi  na  kutufahamisha taarifa  za  msingi  kuhusu  nchi  hiyo."

Deutschland 42.Ordentlicher Bundestag des DFB Oliver BierhoffFestakt,
Meneja wa timu ya taifa ya Ujerumani Oliver BierhoffPicha: picture-alliance/augenklick/firo Sportphoto

Rais  wa  shirikisho  la  kandanda  nchini  Ujerumani  DFB, Reinhard Grindel  amesema,  kwamba  ziara  ya  masaa matatu  ya  Merkel  ilikuwa  ya uwazi  na  iliyofanikiwa sana.  "Alitutakia  kila  la  kheri  na  bahati  njema," aliongeza   nahodha  msaidizi  Sami  Khedira. Ilikuwa mkusanyiko  wa  utulivu  kabisa. Kansela  ambaye  pia alichukua  muda  kusalimiana  na  wapenzi  wa  kandanda nje  ya  hoteli  hakuhusisha  vipingamizi vingi, alionesha utu, mkweli  na  mwenye  hamasa  sana, alisema  Khedira.

 

Mwandishi: Sekione Kitojo / rtre / afpe /dpae

Mhariri: Josephat Charo