ISTANBUL.Papa akutana na kiongozi wa kanisa la Orthodox
30 Novemba 2006Matangazo
Baba mtakatifu Benedikt wa 16 katika ziara yake nchini Uturuki amekutana na kiongozi wa kanisa la Greek Orthodox Bartholomew wa kwanza katika mji wa Istanbul.
Ziara ya baba mtakatifu ina lengo la kuziba ufa baina ya kanisa hilo lililo jitenga kutoka kanisa katoliki takriban mika 1000 iliyopita.
Licha ya kuwepo waumini wachache wa kanisa hilo mjini Istanbul Bartholomew bado anatambuliwa miongoni mwa viongozi wa kwanza wa kanisa hilo la Orthodox.