HANOI: Uhusiano wa kibalozi kuanzishwa kati ya Vietnam na Vatikan
1 Februari 2007Matangazo
Vietnam na Vatikan zinataka kuanzisha uhusiano wa kibalozi.Kwa mujibu wa msemaji wa serikali ya kikomunisti mjini Hanoi,mada hiyo ilijadiliwa wakati wa ziara ya waziri mkuu Nguyen Tan Dung hapo Januari 25,ambapo alikutana na Papa Benedikt wa XVI.Lakini hakusema uhusiano huo wa kibalozi utaanzishwa lini.Katika bara la Asia,baada ya Ufilipino,Vietnam ni nchi yenye idadi kubwa sana ya Wakatoliki,ikiwa ni asilimia 10 ya umma wa Vietnam wa milioni 84.