GAZA: Wapalestina wanne wauwawa na jeshi la Israel
14 Agosti 2007Matangazo
Wanajeshi wa Israel wamewaua wapalestina wanne wakati wa operesheni waliyoifanya leo kusini mashariki mwa Ukanda wa Gaza.
Msemaji wa jeshi la Israel amesema uvamizi huo ulilenga kutafuta mtandao wa mahandaki unaotumiwa na wanamgambo wa kipalestina ili kuzuia maroketi kuvumishwa dhidi ya Israel.
Duru za hospitali zinasema mama mmoja pamoja na mwanawe wa kiume mwenye umri wa miaka 25 wameuwawa na kombora la Israel wakati walipokuwa ndani ya nyumba yao.
Walioshuhudia wanasema watu wengine wasiopungua 11 wamejuruhiwa katika uvamizi huo.