1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Gari lagonga watu Ujerumani, watatu wauawa, 20 wajeruhiwa

Iddi Ssessanga
7 Aprili 2018

Watu wasiopungua wanne wameuawa baada ya basi dogo kuparamia kundi la watu katikakati mwa mji wa Muenster nchini Ujerumani Jumamosi mchana. Habari zinasema dereva wa gari hilo ni Mjerumani mwenye matatizo ya akili.

https://p.dw.com/p/2vf2S
Deutschland Kleintransporter fährt in Münster in Menschenmenge - Tote und Verletzte
Polisi wakifanya ukaguzi katika eneo ambako gari limegonga watu na kusababisha vifo vya wanne na 20 kujerihiwa.Picha: Reuters/NonstopNews

Waliokufa wanahusisha dereva mshukiwa, aliejiuwa kwa kujipiga risasi akiwa ndani ya gari hilo kwa mujibu wa msemaji wa jeshi la polisi.

Lakini gazeti maarufu la Sueddeutsche Zeitung limeripoti kuwa maafisa wanaamini hakukuwa na lengo la ugaidi katika tukio hilo, na kwamba dereva huyo anaaminika kuwa Mjerumani mwenye umri wa kati aliekuwa na matatizo ya kisaikolojia.

Gazeti la Sueddeutsche pia limeripoti kuwa nyumba ya mshukiwa ilikuwa ikakaguliwa kutafuta uwezekano wa kuwepo na viripuzi. maafisa wa serikali ya Ujerumani walikuwa bado hawajasema ni nini wanadhani lilikuwa lengo la tukio hilo.

Na wakati huo huo, polisi walisema walikuwa wanahakiki ripoti za mashuhuda kwamba wahalifu wengine huenda wamekimbia kutoka kwenye gari hilo.

Msemaji wa Polisi Andreas Bode anasema mashuhuda waliwambia kuwa watu wengine waliondoka kwenye gari baada ya kugonga. Shirika la habari la Ujeurmani DPA, liliripoti kwamba mashuhuda walizungumzia juu ya watu wawili waliokuwemo ndani ya basi hilo mbali na dereva.

Deutschland Kleintransporter fährt in Münster in Menschenmenge - Tote und Verletzte
Polisi wakizuwia mtaa ulio karibu na eneo la tukio.Picha: Reuters/NonstopNews

Bode alisema polisi ilikuwa imegundua kifaa cha kutia mashaka ndani ya gari hilo na walikuwa wanakichunguza. Meya wa Muenster alisema maafisa walikuwa bado hawajabaini lengo la tukio hilo. Meya huyo Markus Lewe aliwaambia waandishi habari kwamba Muenster nzima ilikuwa inawomboleza tukio hilo baya.

Maandamano ya Wakurdi

Tayari askari polisi wengi walikuwa katika eneo hilo waklifanya doria wakati wa maandamano ya Wakurdi, na tukio hilo lilitukia muda sawa wa maandamano hayo wa saa tisa na nusu za alasiri.

Wafanyakazi wa mgahawa ulio karibu na baa ambako shambulio hilo lilitokea walielezea kusikia sauti kubwa kabla ya mambo kuanza kwenda haraka na walilaazimika kuondoka mgahawani hapo. Hawakuona tukio halisi litikokea.

Serikali ya Ujerumani imetoa salamu za rambirambi kwa wahanga. "Habari mbaya za Muenster," aliandika msemaji Ulrike Demmer kwenye ukurasa wa twitter.

Waziri wa sheria Katarina Barley alizishuru taasisi za huduma za dharura na kusema kwamba kila kitu kinapaswa kufanyw aili kubaini kilichopelekea tukio hilo. Muenster ni mmoja ya miji muhimu ya vyuo vikuu nchini Ujerumani, ukijivunia zaidi ya wanafunzi 50,000.

Mwandishi: Iddi Ssessanga/dpae, ape,rtre

Mhariri. Yusra Buwayhid