1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

BRUSSELS: Uturuki isishambulie waasi ndani ya Irak

16 Oktoba 2007
https://p.dw.com/p/C7FH

Mpango wa Uturuki kutaka kuchukua hatua za kijeshi dhidi ya waasi wa Kikurd ndani ya ardhi ya Irak unazidi kulaumiwa.Mkuu wa Umoja wa Mataifa anaeshughulikia wakimbizi,Antonio Guterres akizungumza mjini Brussels amesema, hatua kama hiyo itasababisha wimbi la wakimbizi katika kanda ya utata.Umoja wa Ulaya na Marekani kwa mara nyingine tena,zimetoa mwito kwa Uturuki iliyo mshirika wao katika NATO,kutochukua hatua ya kijeshi,kaskazini mwa Irak.