BRAZZAVILLE:Mbirikimo waombwa radhi na serikali
16 Julai 2007Matangazo
Serikali ya Kongo Brazaville inaomba radhi rasmi kwa kuwapa kundi moja la wanamuzi wa mbirikimo malazi kwenye hifadhi ya wanyama kinyume na ilivyowafanyia wanamuziki wengine.
Kulingana na serikali hatua hiyo ilichukuliwa ili kuwaweka katika mahali ambapo wamezoea kwani wanaishi kwenye misitu ya mbali.Magazeti ya eneo hilo na makundi ya kutetea haki zabinadamu wamelaani kitendo hicho kwani kiliwadhalilisha.Serikali iliamua kuwahamisha hadi shule moja.Wanamuziki hao walikuwa wanashiriki katika tamasha la Pan Afrika Music.