BERLIN:Jeshi la Ujerumani kutoa msaada wa kitalaamu zaidi likihitajika
12 Agosti 2007Matangazo
Waziri wa maendeleo wa Ujerumani bibi Heidemarie Wieczorek-Zeul amesema kwamba uwezekano upo wa Ujerumani kutoa mchango zaidi katika harakati za kulinda amani katika jimbo la Darfur nchini Sudan.
Kwa sasa Ujerumani inashughulikia maswala ya kilojistiki ya usimamizi na mikakati ya usafirishaji kwa ndege katika jimbo la Darfur nchini Sudan.
Jeshi la Ujerumani Bundeswehr lina mamlaka ya kubakia katika jimbo la Darfur hadi katikati ya mwezi Desemba na linaweza kutoa mchango wa wataalamu wake wa kijeshi hadi kufikia mia 200 katika kukisaidia kikosi cha umoja wa Afrika huko magharibi mwa Sudan.