1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Berlin. Uchumi wa Ujerumani kuongezeka mwakani.

24 Desemba 2006
https://p.dw.com/p/CCgZ

Waziri wa uchumi wa Ujerumani Michael Glos amesema anatarajia ukuaji zaidi wa uchumi katika mwaka 2007 kuliko hapo kabla ilivyofikiriwa.

Glos ameueleza hali ya uchumi nchini Ujerumani kuwa ni bora kuliko wakati mwingine wowote tangu mataifa mawili ya Ujerumani kuungana na amesema kuwa anafikiri hali hiyo italeta hali bora katika soko la kazi la nchi hiyo katika mwaka ujao.

Ujerumani imekuwa ikitarajia ukuaji wa asilimia 1.4 katika mwaka 2007.