1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

BERLIN : Rais wa Ujerumani alikuwa akipelelezwa

25 Novemba 2006
https://p.dw.com/p/CCpN

Gazeti la Ujerumani la Der Spiegel limeripoti kwamba Wizara ya Usalama ya Ujerumani Mashariki Stasi kwa miaka mingi imekuwa ikimpeleleza Rais wa sasa wa Ujerumani Horst Köhler.

Kupelelezwa huko kwa Kohler kumefanyika wakati akiwa muajiriwa wa wizara ya fedha.

Rais huyo amesema amekuwa akifahamu juu ya kufichuliwa kwa taarifa hizo za ujasusi kwa wiki kadhaa sasa na tayari ameliangalia jalada lake la Stasi.