1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

ACCRA:Umoja wa mataifa ya Afrika kujadiliwa

2 Julai 2007
https://p.dw.com/p/CBmb

Viongozi wa Umoja wa Afrika wanaokutana mjini Accra nchini Ghana wanajadilia mipango ya kuwa na Muungano wa Mataifa ya Afrika ulio na lengo la kuondoa suala la mipaka baina ya mataifa.Hiyo ndiyo mada rasmi katika ajenda ya mkutano huo ulioingia siku yake ya pili.Pembezoni mwa suala hilo viongozi hao aidha wanatarajia kujadilia matatizo yanayoyumbisha Bara la Afrika hususan eneo la Darfur na Zimbabwe.

Maandamano yamepigwa marufuku hadi siku ya mwisho ya kikao hicho cha siku tatu.Polisi alfu mbili wanashika doria mjini humo.