Zanzibar na swala la eneo la Bahari ya Hindi
23 Januari 2012Matangazo
Wajumbe wengi wa baraza la wawakilishi visiwani Zanzibar wametaka Waziri wa maliasili wa Zanzibar Juma Shamhuna ajiuzulu. kufuatia sakata la kushirikiana kinyemela na serikali ya jamhuri ya muungano wa Tanzania kufanikisha ombi la kutaka nyongeza ya eneo la bahari ikijumuisha mipaka ya visiwa hivyo, pasipo kulishauri baraza hilo.Wito wa kutakiwa kujiuzulu kwa waziri huyo mkongwe visiwani Zanzibar unafuatia hoja binafsi iliyotolewa na mwakilishi wa Jimbo la Mji Mkongwe Ismail Jussa. Kufutia hali hiyo Sudi Mnette alizungumza na Issa Yusuf, Mwandishi kutoka Zanzibar kujua ni yapi yaliyojitokeza hadi wakati huu .
Mwandishi: Sudi Mnette
Mhariri: Saumu Mwasimba