Waziri wa misaada ya maendeleo wa Ujerumani ziarani Aceh
16 Desemba 2006Matangazo
Banda Aceh:
Waziri wa misaada ya maendeleo wa serikali kuu ya Ujerumani bibi Heidemarie-Wieczoreck-Zeul analitembelea jimbo la Aceh nchini Indonesia,miaka miwili baada ya janga la Tsunami kupiga katika eneo hilo.Mkurugenzi wa idara ya ujenzi mpya,Kuntoro MANGKUSUBROTO,amemuelezea jinsi shughuli za ujenzi mpya,zinazogharimiwa zaidi kwa msaada wa maendeleo wa Ujerumani zinavyoendelea.Hii leo waziri Heidemarie Wieczoreck-Zeul analitembelea kwa helikopta eneo hilo la maafa.Watumishi kadhaa wa mashirika ya misaada ya maendeleo ya ujerumani wanasaidia katika jimbo la Aceh,ikiwa ni pamoja na watumishi wa shirika la misaada ya kiufundi na jumuia ya ushirikiano wa kiufundi GTZ.