1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Waziri mkuu wa Somalia aapishwa

24 Novemba 2007
https://p.dw.com/p/CSks

Bunge nchini Somalia limemuapisha waziri mkuu mpya, Nur Hassan Hussein hii leo, likiwa na matumaini ya kuiimarisha serikali ya mpito ambayo imedhoofishwa na mkwamo wa kisiasa na vita dhidi ya wanamagambo.

Nur Hassan aliyeteuliwa mapema juma hili ameapishwa baada ya wabunge 211 kati ya wabunge 212 kumuidhinisha huko mjini Baidoa, makao makuu ya serikali ya mpito ya Somalia.

Hussein ameahidi ataiongoza Somalia kwa uaminifu na atafanya kila awezalo kuiimarisha.