1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Watu 11 wauwawa katika mapigano makali Mogadishu.

Mohamed Dahman8 Juni 2008

Watu 11 wameuwawa leo hii katika mapambano makali kati ya wanajeshi wa Ethiopia wakishirikiana na wale wa serikali ya Somalia dhidi ya waasi wa siasa kali za Kiislam mjini Mogadishu.

https://p.dw.com/p/EFfu
Mwanajeshi wa serikali ya mpito nchini Somalia.Picha: AP

Kwa mujibu wa mashahidi vikosi vya serikali vikiiungwa mkono na vile vya Ethiopia vilifanya msako katika mtaa wa Wardhigley kusini mwa mji mkuu wa nchi hiyo Mogadishu na kuzusha mapigano ambapo mahasimu walishambiliana kwa kutumia silaha nzito

Waethiopia walifyetua mizinga katika soko la Bakara ambapo inaelezwa kwamba raia wengi waliuwawa.Wanajeshi watatu wa Somalia na mwanamgambo mmoja wameuwawa katika kitongoji cha karibu cha Hararyale ambapo mpigano yaliwa makali sana.

Vikosi vya Ethiopia na vya Somalia pia vimekuwa vikitumia silaha za kutungulia ndege katika mapigano hayo.