Wakulima masikini wagundua njia ya kuondosha ujinga
Veronica Natalis5 Agosti 2015
Wakati wakaazi wa maeneo mengine nchini Tanzania wakingojea serikali kuwajia na majibu ya kila tatizo lao, mkoani Shinyanga wananchi wamegundua njia ya kujipatia ufumbuzi wa matatizo yao wao wenyewe, wakianzia na kuanzisha kituo cha kujisomesha na kujisomea vitabu.