Serikali ya Kenya imetangaza amri ya kutotoka nje usiku katika mtaa wa mabanda wa Kibera, baada ya wafuasi wa upinzani kuandamana kutaka viongozi wao waliokamatwa kuhusiana na matamshi ya chuki waachiliwe huru. Wakati huo huo mawakili wa upinzani CORD wako mahakamani kuwasilisha ombi la wabunge hao waachiliwe kwa dhamana.