1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wahariri wa magazeti watoa maoni juu ya Ujerumani kuipa Israel nyambizi

Abdu Said Mtullya5 Juni 2012

Wahariri wa magazeti leo wanazungumzia juu ya mgogoro wa madeni barani Ulaya na suala la Ujerumani kuipa Israel nyambizi. Pia wanatoa maoni juu ya Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza.

https://p.dw.com/p/158AB
Nyambizi aina ya Dolphin,iliyotolewa na Ujerumani kwa Israel
Nyambizi aina ya Dolphin, iliyotolewa na Ujerumani kwa IsraelPicha: Reuters

Juu ya mgogoro wa madeni gazeti la "Neue Presse" linasema kwamba sasa linahitajika suluhisho la Ulaya, yaani sera ya kiuchumi ya pamoja na hatimaye umoja wa kisiasa. Na hatua ya pili ni kwa nchi zote za Umoja wa sarafu ya Euro kushikamana ili kuyakabili madeni.

Gazeti la "Wiesbadener Kurier" linatilia maanani kwamba katika  juhudi za kuukabili mgogoro wa madeni mabenki yamepunguza mikopo.Mhariri wa gazeti hilo  anaeleza kwamba mabenki yamepunguza mikopo kwa kiwango kama kile, baada ya benki ya Lehman kusambaratika. Hiyo ni ishara ya mbiu ya mshikamano wa eneo la Umoja wa sarafu ya Euro. Nchini Ujerumani dalili za mabenki kuipunguza mikopo bado hazijaonekana. Hatahivyo uchumi  wa Ujerumani umezingwa zingwa  katika uekezaji vitega uchumi. Kinachopasa kufanya sasa ni  kusubiri ishara thabiti kutoka  Marekani na China. Pia inapasa kusubiri kuona jinsi wagiriki watakavyopiga kura. Lakini haidhuru matokeo hayo yatakuwaje, mustakabal wa sarafu ya Euro unahitaji msingi imara wa umoja wa  kisiasa barani Ulaya.

Gazeti la "Mitteldeutsche Zeitung" linazungumzia juu ya uamuzi wa Ujerumani wa kuipa Israel nyambizi inayoweza kutumia silaha za nuklia. Mhariri wa gazeti hilo anaeleza sababu ya Ujerumani kuupitisha uamuzi huo.  Israel ni nchi yenye eneo dogo sana. Ndiyo kusema inaweza kuteketezwa kwa mabomu machache tu ya nyuklia. Na kwa hivyo ili kujihami inahitaji kuwa na nyambizi ya nyukulia  ili kuwafanya maadui zake asilani wasithubutu kuishambulia. Huo ndio utakuwa usalama wa  uhakika kwa Israel, endapo nchi ya  kiadui kama Iran siku moja itamiliki  bomu la nyuklia.Kwa hiyo hatua ya Ujerumani ya kuipa  Israel nyambizi, siyo uamuzi wa kuipa nchi hiyo  silaha ya kivamizi.


Malkia Elizabeth wa 2 ameadhimisha miaka 60 ya utawala wake nchini Uingereza.Katika muda huo wote Malkia huyo ameonyesha nidhamu ya hali ya juu. Lakini gazeti la "Badische Neueste Nachrichten" linauliza jee ni mpaka lini, na linasema kuwa Malkia Elizabeth ameonyesha nidhamu thabiti.Wakati wote amejihesabu kuwa ni mtumishi wa nchi.Katika nyakati za migogoro kama sasa ni jambo la kutia moyo kuona msimamo kama huo.Lakini sasa limebakia swali,jee ni mpaka lini. Uingereza pia haipo nje ya nyakati. za dunia

Mwandishi:Mtullya Abdu/

Duetsche Zeitungen/

Mhariri:  Othman,Miraji