Waalgeria wapinga machafuko
9 Septemba 2007Matangazo
ALGIERS:
Kiasi cha Waalgeria 5000 walikusanyika leo katika kitovu cha mji mkuu Algiers kulalamika juu ya machafuko ya umwagaji damu yaliochukua maisha ya watu 57 humo nchini.
Tawi la Afrika ya kaskazini la Al Qaeda,limesema ndilo lenye jukumu la mashambulio 2 moja kati ya hayo lililengwa dhidi ya rais Abdel Aziz Bouteflika.