1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Putin: Nitakuja Korea kaskazini kuimarisha uhusiano wetu

Lilian Mtono
14 Septemba 2023

Rais wa Urusi Vladimir Putin amekubali mwaliko wa kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un wa kuletembelea taifa hilo.

https://p.dw.com/p/4WKnx
Rais wa Urusi Vladimir Putin akiwa na kiongozi wa Korea kaskazini Kim Jong Un
Rais wa Urusi Vladimir Putin akiwa na kiongozi wa Korea kaskazini Kim Jong UnPicha: Sputnik/Mikhail Metzel/Kremlin via REUTERS

Kulingana na shirika la habari la serikali ya Pyongyang, Kim alitoa mwaliko huo baada ya mazungumzo na Putin katika Jukwaa la Uchumi kwa Mataifa ya Mashariki, mjini Vladivostok.

Jana Jumatano, Kim aliapa kuisadia Moscow kwa kila hali katika vita vyake nchini Ukraine, matamshi yaliyokosolewa vikali na Marekani pamoja na katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres akiyataka mataifa hayo kuheshimu maazimio ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.

Soma pia:Rais Putin akubali mwaliko wa Kim Jong Un

Marekani ilisema jana inaufutilia mkutano baina ya wakuu hao wawili kwa karibu na kuionya Korea Kaskazini kwamba itakabiliwa vikali ikiwa itamsaidia Putin.