Vyombo vya habari
Uhuru wa vyombo vya habari haujakomaa
2 Mei 2017Matangazo
Huku dunia ikiadhimisha siku ya uhuru wa habari , waandishi habari nchini Uganda wanazidi kukabiliwa na mazingira magumu ya kazi kutokana na sheria kandamizi zinazobuniwa kila kukicha. Aidha makabiliano na vyombo vya usalama hasa polisi na vitisho vya mara kwa mara kutoka kwa wanasiasa na hata waajiri wao vimeshudiwa mara kwa mara. Haya ni licha ya madai ya utawala nchini humo kwamba unalinda kwa dhati uhuru wa habari.