1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Uganda: Mkutano wa Kimataifa kutoka kanda ya maziwa makuu wafanyika Kampala

Samia Othman6 Agosti 2012

Mkutano wa Kimataifa wa viongozi wa Afrika kutoka kanda ya maziwa makuu umeanza leo jijini Kampala, Uganda.

https://p.dw.com/p/15kYo
Rais Yoweri Museveni wa Uganda
Rais Yoweri Museveni wa UgandaPicha: AP

Mkutano huo utajadili kwa kina mzozo unaoendelea katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na namna ya kupata suluhu juu ya mzozo huo, ikiwemo kuundwa kwa kikosi cha kimataifa cha kulinda amani na kupambana na waasi wa M23 wanaoyumbisha amani ya DRC.

Mkutano huo unajumuisha nchi 11, zikiwemo Angola, Burundi, Congo, Kenya, Rwanda, Sudan,Tanzania, Zambia na mwenyeji, Uganda.

Mwandishi wetu Saleh Mwanamilongo anahudhuria mkutano huo na Amina Abubakar amezungumza naye na mwanzo anatupa hali halisi ya mambo katika mji huo.

(Kusikiliza mazungumzo hayo bonyeza alama ya spika za masikioni hapo chini)

Mwandishi Amina Abubakar

Mhariri Othman Miraji