1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Uefa Euro 2012: Timu zafanya maandalizi ya mwisho

4 Juni 2012

Uingereza inafanya jaribio la mwisho hii leo kabla ya kuingia dimbani katika fainali za kombe la mataifa ya Ulaya, Euro 2012, wakati kocha wa Ujerumani Joachim Loew asema kikosi chake kinahitaji marekebisho makubwa.

https://p.dw.com/p/156vs
epa03204565 (FILE) The mascots of the UEFA EURO, Slavek (L) and Slavko (R), pose in the Donbass Arena stadium during their presentation in Donetsk, Ukraine, 23 November 2010. The stadium in Donetsk will host three preliminary round games, one quarter final and one semi final of the UEFA EURO 2012. EPA/PHOTOMIG *** Local Caption *** 00000402463512 +++picture alliance / dpa
Alama ya fainali za EURO 2012Picha: picture-alliance/dpa

Uingereza inakwaana na Ubelgiji huku kukiwa na taarifa za majeruhi kadha katika kikosi cha kocha Roy Hodgson. Hali ya wasi wasi tayari imetanda katika kambi ya Uingereza kufuatia hatua zisizokuwa na utaratibu mzuri za maandalizi katika mashindano haya baada ya kupata pigo mara mbili kwa kumpoteza Gareth Barry na Frank Lampard baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Norway.

Euro 2012 Qualifying - Group G England v Wales 26 March 2011. England pose for a team photo before kick off Photo: Javier Garcia / BPI
Kikosi cha timu ya taifa ya Uingereza Euro 2012Picha: picture-alliance / Back Page Images

Kuwapoteza wachezaji hao wazoefu wa kati kunakiweka kikosi hicho cha kocha Roy Hogdson kuwa finyu zaidi katika eneo hilo, wakati jukumu la nahodha Steven Gerrard na Scott Parker kupata umuhimu zaidi.

Uingereza inafungua mchezo wa kundi D dhidi ya Ufaransa Juni 11, na Hogdson anaweza kusameheka kwa kuwalinda wachezaji wake hao wa kati hadi pale mambo yatakapokuwa hadharani katika uwanja wa Donbass Arena huko Ukraine.

Ureno imo mbioni katika kukinoa kikosi chake pamoja na kurekebisha mbinu hapa na pale kabla ya kuingia dimbani kuumana na Ujerumani. Baada ya sare za bila kufungana dhidi ya Poland na hivi karibuni kutoka sare na Macedonia, Christiano Ronaldo na kundi lake wanataka kupata goli lao la kwanza tangu kikosi hicho kilipoirarua Bosnia- Herzegovina mabao 6-2 katika mchezo wao wa marudio katika kundi B, wakati Ureno inakwaana na Uturuki mjini Lisbon.

Kocha wa Ureno Paulo Bento amesema .

Portugal's soccer team head coach Paulo Bento talks to journalists during a news conference Friday, May 4, 2012, at the Portuguese Soccer Federation headquarters in Lisbon. On Thursday the Federation announced it had extended Bento's contract until 2014.( AP Photo / Joao Henriques )
Kocha wa Ureno Paulo BentoPicha: AP

"Lengo letu la kwanza ni kufikia nusu fainali ya kombe la mataifa ya Ulaya .Baada ya hapo tutaangalia mchezo baada ya mchezo itakuwaje katika michezo yetu mitatu ya mwanzo. Tunatambua kuwa tumo katika kundi gumu, lakini tunataka tunataka kuingia katika nusu fainali kwanza ya kombe la Ulaya".

Kikosi cha kocha Bert van Marwirjk kitaingia dimbani leo jioni kukwaana na Ireland ya kaskazini mjini Amsterdam, leo siku saba kabla ya kutiana kifuani na Denmark mabingwa wa mwaka 1992 wa kombe hilo la mataifa ya Ulaya.

Lakini kocha wa Ujerumani ambaye hivi sasa anakinoa kikosi chake kisaikolojia na mbinu, amekiri kuwa timu yake inahitaji kufanya kazi ya ziada baada ya kusumbuka kwa muda wa dakika 90 na kupata ushindi mwembamba wa mabao 2-0 dhidi ya Israel ambayo inaonekana kuwa dhaifu, katika mchezo wao siku ya Alhamis.

Germany's national soccer team coach Joachim Loew reacts during his team's international friendly soccer match against Switzerland at St Jakob Park stadium in Basel, May 26, 2012. REUTERS/Michael Buholzer (SWITZERLAND - Tags: SPORT SOCCER)
Kocha wa Ujerumani Joachim LoewPicha: Reuters

"Ulikuwa , naweza kusema , mchezo wa kawaida wa majaribio na mtu anaweza kusema katika baadhi ya nyakati kuwa mambo mengi hayakwenda sahihi. katika kipindi cha pili tuliweza kushirikiana vizuri zaidi na kuonyesha lengo letu.Lakini wakati tunaingia katika wiki ya mwisho, na ushindi huu , unatoa nguvu kwa timu yetu".

Italy coach Cesare Prandelli leads a training session ahead of Friday's Euro 2012 soccer qualifier against Northern Ireland, at the Coverciano sports center, near Florence, Italy, Thursday, Oct. 7, 2010. (AP Photo/Fabrizio Giovannozzi)
Kocha wa Italia Cesare PrandelliPicha: AP

Wakati huo huo Italia inasema kuwa itajitoa katika fainali za kombe la mataifa ya Ulaya iwapo itaombwa kufanya hivyo kwa manufaa ya mchezo wa kandanda, amesema kocha Cesare Prandeli jana Ijumaa baada ya madai ya kashfa ya kupanga matokeo kuchafua jina la kikosi cha Squardra Azzurri timu ya taifa ya Italia.

Mawandishi: Sekione Kitojo,

Mhariri: Mohammed Abdul-Rahman