Kulingana na ripoti ya Umoja wa Mataifa, Rwanda imewaandikisha na kuwapatia mafunzo ya kijeshi wakimbizi kutoka Burundi miongoni mwao wakiwemo watoto. Kwa lengo kuu la kumuondowa madarakani Rais Piere Nkurunziza. Mtaalamu wa masuala ya usalama kutoka Kenya, Semiyu Werunga, anaeleza mtazamo wake.