1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

TOKYO: Kimbunga Man Yi chavuma visiwani Okinawa

13 Julai 2007
https://p.dw.com/p/CBj9

Kimbunga kikali kimevuma katika visiwa vya Okinawa,kusini mwa Japan.Zaidi ya watu 100,000 wamebakia bila ya umeme na idadi fulani ya nyumba zimesombwa na mvua kubwa zilizosababishwa na kimbunga Man-Yi.Vile vile zaidi ya watu 8,000 wameshauriwa kuhamia kwengineko.Kama safari 400 za ndege zimefutwa.Siku ya Jumamosi,kimbunga hicho kinatazamiwa kufika magharibi ya Japan kwenye kisiwa cha Kyushu,ambako tayari maelfu ya watu wamehamishwa sehemu zingine.