1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

TOKYO: Kansela Merkel akamilisha ziara ya Bara Asia

31 Agosti 2007
https://p.dw.com/p/CBUG

Kansela wa Ujerumani,Angela Merkel leo Ijumaa anakamilisha ziara yake nchini Japan.Mjini Kyoto leo mchana,Merkel atatoa hotuba muhimu kuhusu tatizo la kuongezeka kwa kiwango cha joto duniani.

“Itifaki ya Kyoto“ kuhusu njia za kupambana na mabadiliko ya hali ya hewa duniani,ilitiwa saini miaka kumi iliyopita mjini Kyoto.

Kansela Merkel,kutoka Kyoto ataelekea Osaka kuhudhuria Mashindano ya Riadha Ulimwenguni na atarejea Ujerumani siku ya Jumamosi.